Mahakama ya Wilaya ya Nicosia Yasitisha Hukumu

Desemba 2, 2014

 Jaji katika Mahakama ya Wilaya amesitisha hukumu kufuatia hati ya ziada ya wanahisa wa FBME tarehe 1 Desemba, baada ya kusikiliza maelezo ya mdomo na ya maandishi kuhusu kufungua jalada kwenye mahakama ya usuluhishi ya Kimataifa ya Biashara mjini Paris. Kama ilivyo kawaida ya taratibu za kimahakama, amesitisha hukumu hadi tarehe ya baadae juu ya maombi ya muda mfupi ya wanahisa kuzuia uuzaji wa amana za tawi la FBME la Cyprus na kuzuia hatua za Msimamizi wa Benki Kuu ya Cyprus zenye kuharibu zaidi biashara ya Benki hiyo.