Heri ya Krismasi na Mwaka Mpya

Desemba 16, 2014

Katika msimu huu wa sikukuu, wanahisa wa Benki ya FBME wanawapa salamu na kuwatakia heri wateja wote, wafanyakazi, washirika wetu na familia zao na wengine wote wenye nia njema kwa ajili ya Krismasi na Mwaka Mpya.

Miezi hii iliyopita kumekuwa na matatizo mengi yasiyotarajiwa kwa wasio na hatia. Baadhi wamepoteza ajira zao, wengine wameshindwa kupata fedha zao, ikiwa ni pamoja na wengi waliotaka kulipa mishahara na gharama za uendeshaji kwenye biashara zao. Makampuni yamefungwa na watu binafsi, familia zao na marafiki zao wanapata msongo wa mawazo wa kutojua ni kipindi kipi chenye furaha katika mwaka. Kutokana na mazungumzo yetu na wateja, wafanyakazi na wengine, tunaamini kwamba watu takribani 100,000 wameathirika na uamuzi wa Benki Kuu ya Cyprus wa kulazimisha hatua za Azimio dhidi ya tawi la FBME Cyprus

Wanahisa pia wanawatakia heri wananchi wote wa Cyprus ambao wamekuwa waathirika wasio na hatia wa vitendo potofu kwa Jamhuri.
Kwa kila mmoja, tunatarajia mwaka wenye mabadiliko wa 2015!